Ninawezaje kupangilia majina ili kuepuka kosa la "Inahitaji taarifa zaidi" wakati wa kushikia nafasi ibada?

Share

Ili kushikia nafasi jina la babu kwa ajili ya ibada za hekaluni, lazima kwanza uhakikishe kwamba jina lake lina mpangilio ulio sahihi katika Mti wa Familia. Kama sivyo, unapokea ujumbe ukikuambia kwamba taarifa zaidi inahitajika. Kupangilia kwa usahihi jina la babu yako kunaweza kukutatanisha, hasa wakati unapokuwa unajua sehemu tu ya jina hilo. Jifunze nini cha kufanya wakati jina kamili halijulikani. 

Majedwali hapa chini yanatoa mifano ya mipangilio halali na batili ya majina kwa ajili ya ibada za hekaluni. 

Jedwali 1: Unajua jina la mume, lakini jina la mke halijakamilika. 

CheoMajina ya KwanzaJina la MwishoLinastahiliMuhtasari
 Amy NdiyoWakati jina la ukoo la mke linapokuwa halijulikani na pako wazi.
Bi.*JeffFrazierNdiyoJina linastahili ikiwa jina la Bi. linafuatiwa na jina la mume katika uga sahihi.
ClarkNdiyoJina la ukoo la mke linajulikana, na jina la kwanza halijulikani.
Bi. Jeff FrazierHapanaTenganisha jina katika sehemu tofauti. Sehemu haziwezi kuunganishwa katika uga.
Bi. Jeff FrazierHapana
Bi. JeffFrazierHapana
Bi.Jeff FrazierHapana
Bi.Hapana
Bi.Hapana
Bi.FrazierHapana

*Inajumuisha Bi., Bi, na yaliyo sawa katika lugha zote.

Jedwali 2: Unajua jina la mmoja wa wazazi, lakini jina la binti halijakamilika. 

CheoMajina ya KwanzaJina la MwishoLinastahiliMuhtasari
Bi*DonnaFrazierNdiyoHili linastahilishwa na kichwa cha Bi
FrazierNdiyoWakati jina la kwanza linapokuwa halijulikani, usiongezee cheo.
Bi. DonnaFrazierHapanaTenganisha jina katika sehemu tofauti. Sehemu haziwezi kuunganishwa katika uga.
Bi. FrazierHapana
Bi. FrazierHapana
Bi.FrazierHapanaCheo kisicho na jina la kwanza ni batili.
Bi.FrazierHapanaBi. sio jina halali la kwanza.
Bi.Hapana

*Inajumuisha Bi. na yaliyo sawa na hayo katika lugha zote.

Jedwali 3: Unajua jina la mmoja wa wazazi, lakini jina la mwana halijakamilika. 

CheoMajina ya KwanzaJina la MwishoLinastahiliMuhtasari
Bwana*JohnFrazierNdiyoHili linastahili kuwa na cheo cha Bwana.
FrazierNdiyoWakati jina la kwanza linapokuwa halijulikani, usiongezee cheo.
Bw. JohnFrazierHapanaTenganisha jina katika sehemu tofauti. Sehemu haziwezi kuunganishwa katika uga.
Bwana FrazierHapana
Bw. FrazierHapana
Bw.FrazierHapanaCheo kisicho na jina la kwanza ni batili.
BwanaFrazierHapanaBwana si jina halali la kwanza.
MrHapana

*Inajumuisha Bwana, Bw., na yaliyo sawa na hayo katika lugha zote.

Kumbuka: Kuwa makini kwamba hauongezi maneno yoyote ambayo si sehemu ya jina halisi la mtu—maneno kama "yasiyotajwa," "Mama," "Mume," au "Shangazi." Haya yatakuzuia wewe kushikia nafasi jina na kusababisha upokee ujumbe unaoomba taarifa zaidi. 

Kama utaingiza alama ya swali badala ya jina la mtu katika Mti wa Familia, ibada zake zinaonyesha kama "Inahitaji taarifa zaidi." Hakuna kazi ya ibada inayoweza kufanyika mpaka jina linapopatikana na kuingizwa.

Makala zinazohusiana

Ni maneno na vifupisho gani vinasababisha maneno "Inahitaji taarifa zaidi" kuonekana?
Ni kwa jinsi gani ninapaswa kuingiza majina katika Mti wa Familia?
Katika Mti wa Familia, je, "Taarifa zaidi inahitajika" inamaanisha nini?

moduleTitle